Monday 26 January 2009

habari za TV ya taifa kwa ufupi bila picha

Semaine - mère enfant

Wiki mahsusi kwa ajili ya mzazi na mtoto imeanzishwa leo 26-29/01/2009 nchini kote,ambapo katika mji mkuu bujumbura imeandaliwa kwenye vituo 37 kwa min ajili ya kuwapatishia watoto chanjo dhidi ya maradhi ya kupooza viungo(Polio) pamoja na minyoo ya tumboni.


Elie HARINDAVYI.

VTR :
DP :


















Visite / louis Michel à Gaza

Kamisaa wa umoja wa ulaya anaehusika na misaada ya bin adam duniani louis michel yu ziarani katika ukanda wa gaza kushuhudia pekee namna ya utoaji misaada kwa raia wnaokabiliwa na uhaba wa chakula na dawa.

Pamoja na hivo, kamisaa huyo ameziita pande zinazogomba kuafiki kwa pamoja katika usitishaji mapambano kuwawezesha raia kueshi katika hali tulivu na salama.



NTAMBA Kongo. R

VTR :
DP :











Procès de thomas LUBANGA

Kesi inayomkabili thomas Lubanga kuhusika kuwatumia vijana wenye umri mdogo katika vita kwenye eneo la ituri nchini RDC imesikika kwa mara ya tena mjini la haye nchini uholanzi.



NTAMBA Kongo R.

VTR :
DP :

















INDE / fête nationale

Miaka 59 imetimia kititi leo toka nchi ya india iupate uhuru wake 1950.

Sherehe hiyo inaendeshwa katika hali ya tahadhari kufuatia usalama mdogo unaoendelea kuarifiwa nchini hapo, kutokana na jaribio la kujitoa muhanga lililoendeshwa katika mji wa Bombay miezi 2 iliopita 2009.

Watu zaidi ya 172 waliuwawa wakati wa shambulio hilo lililotafsiriwa kuwa la kigaidi nchini hapo.


NTAMBA Kongo R.


VTR:
DP:










FORUM /consolidation de la Paix (Voix off )

Kudumisha amani ni jukumu la kila raia sehemu aliopo,ikiwa njia pekee itakayopelekea nchi ya Burundi kusalia katika hali tulivu na salama, hasa kufuatia kusainiwa mikataba ya amani kati ya kundi la FNL lililokuwa limesalia kuwa tishio katika mpango mzima wa kudumisha nchini kote Burundi.

Hayo yamo katika juhudi za kuendeleza mijadala tofauti ilio na shabah ya kuirejesha nchi hii kusalia shwari kama zamani, makamu wa pili Yves SAHINGUVU alizinduwa shuhuli ya kudumisha mpango huo utakao husika kwa ujumla namna ya kuheshimu haki za bina dam pamoja na kubuniwa tume itakayo fuatilia uchaguzi ujao wa 2010.


Voix off.

No comments: